Friday, April 20, 2012

ENYI WANAWAKE MSINILILIE MIMI.


ENYI WANAWAKE MSINILILIE MIMI.

 Na; Patrick Samson Sanga.
Kwa nini Yesu aliwaambia akinamama jililieni nafsi zenu na watoto wenu ?
Luka 23:27-28 “Na mkutano mkubwa wa watu wakamfuata na wanawake waliokuwa wakijipiga vifua na kumwombolezea, Yesu akawageukia,akasema,Enyi binti za Yerusalemu ,msinililie mimi,bali jililieni nafsi zenu na watoto wenu”.
Hapa Bwana wetu Yesu alikuwa njiani kuelekea Golgotha kusulubiwa, akina mama na binti za Yerusalemu wakawa wanamlilia na kumwombolezea Yesu kwa uchungu sana.
Sasa kwa kawaida mtu anapokuwa anapita kwenye hali ngumu au matatizo au msiba au janga lolote zito kwa kawaida tunapenda watu wengine watufariji na waomboleze pamoja na sisi na ndiyo maana hata Paulo alisema lieni pamoja na wanao lia nk
Lakini jambo hili halikuwa hivyo kwa Yesu ,kile kilio cha wale akina mama kilimfanya Yesu awageukie na kutoa ujumbe wa ajabu kwa wale akina mama na ndipo akasema msinililie mimi,bali jililieni nafsi zenu na watoto wenu .
Nimeandika ujumbe huu mfupi ili kujibu maswali mawili ambayo tunayapata kutoka katika sentensi ya Bwana wetu Yesu kwa hawa wamama nayo ni;
Moja, kwa nini Yesu aliwaambia msinililie mimi ? mbili kwa nini Yesu aliwaambia jililieni nafsi zenu na watoto wenu?. Yesu aliwaambia msinililie mimi kuu mbili nazo ni;
{a}Ili neno liweze kutimia.Yohana 3:16. Mapatano ya Yesu na baba kule mbinguni ilikuwa Yesu aje na afe  kwa ajili ya watu wake. Ili mlazimu Yesu kupita kwenye hiyo njia, hata kama wangeombolezaje kilio chao kisingeweza zuia kifo cha Bwana Yesu.
Kumbuka kule Gethsemane Ysu mwenyewe aliomba akasema Baba, ikiwezekana kikombe hiki kiniepuke, Lakini tunaona Mungu alituma malaika kumfariji na kumtia moyo na Yesu mwenyewe alikuwa tayari mapenzi ya Mungu yatimizwe.
{b} Kilio chao kingemhuzunisha na kumvunja moyo zaidi. Matendo ya Mitume 21:9-14.Hapa ulikuwa umetolewa unabii wa jinsi vile Paulo atakavyouawa kule Yerusalemu. Na watu wa nyumba ile wakaanza kulia na kumsihi Paulo asipande kwenda Yerusalemu, Ndipo Paulo akawaambia mnafanya nnini, kulia na kunivunja moyo?. Kwa hiyo hata Yesu angekutana na hali ka,a ya Paulo.
Swali la pili; Kwa nini Yesu aliwaambia wamama bali jililieni nafsi zenu na wato wenu na Je alikuwa ana maana gain kuwaambia hivyo?
 Kabla sijakuambia hizo sababu, ngoja kwa kifupi nikuambie habari za nafsi. Kwa kiyunani inaitwa (psuche).Nafsi inahusika kuelekea ndani ya mtu.Ndani ya nafsi ndiko kwenye hisia,akili na maamuzi ya mtu.Hivyo nafsi ya mtu inahusika na maauzi, hisia na nia za mtu binafsi. Nafsi inatabia ya kuugua,kuinama, na na kuumia pale inapojeruhiwa.
Siku zote nafsi inagojea mwongozo wa roho au mwili wa mtu. Mtu akiwa ni wa rohoni nafsi itakaa mkao wa rohoni na mtu akiwa ni wa mwilini na nafsi yake itakaa mkao wa mwilini.Nafsi inaishi sasa kwa kutegemea maneneo unayojisemea au kusemewa na wengine sasa au wakati uliopita.Hivyo Yesu alipowaambia wale kinamama msinililie mimi alikuwa na maana hii na sababu hizi;
*Moja, Yesu alijua akinamama wengi ni watu ambao nafsi zao ni rahisi kujeruhika na kuinama pindi wanapokutana na matatizo mbalimbali na zaidi kina mama wengi ni watu ambao ni wepesi sana kuijtamkia maneno ambayo kwa namna moja au nyingine yanajeruhi nafsi na kuharibu future yao wenyewe.
Kwa Kujua kwamba akina mama wengi mara nyingi huwa wanajitamkia maneno ambayo yanaathari kwao wenyewe, watoto wao, familia zao, kanisa lao na hata nchi nk ndio maana Yesu alisema jililieni nafsi zenu.
 Alikuwa akimaanisha nini?
Yesu alikuwa anawaambia wale wamama wajitunze nafsi zao na za watoto wao kwa kuhakikisha ndani wanweka neno la Mungu linalozungumzia maisha yao ya baadae (future).
Hili neno litazifanya hisia zao, na akili zao na maamuzi yawe yatawaliwe na ahadi za Mungu na hii itawasaidia nafsi kutokuinama wala kujeruhika pindi wanapokutana na matatizo mbalimbali. Neno hili litawapa jibu la kukabiliana na mazingira ya kila nmana kwa sababu hiyo Jehanamu itakosa watu .
*Mbili ni kwa sababu ya nafasi na wajibu ambao Mungu amewapa akinamama kama walinzi wa kusudi lake popote pale walipo.
Nisikilize mwanamke Mungu amekuheshimu sana kukupa wajibu wa kulinda agano na kusudi lake duniani.Shetani anapotaka kuvuruga na kuharibu kusudi la Mungu mahali popote pale, uwe na uhakika lazima tu ataanza kutafuta njia na mpenyo kwa mwanamke.Shetani akitaka kuleta vurugu kwenye ndoa,kanisa,familia uwe na uhakika atafanya kila analoweza apitie kwa mwanamke.
Hebu chukua dakika moja tafakari vile shetani anavyovuruga vijana wa kike na wa kiume, kwa kuwafanya mabinti watoe mimba na kuua bila hata hofu kwa Mungu, Wazazi kufanya tendo la ndoa na wanao, ndugu kwa ndugu, Yesu aliona huzuni na kilio kikubwa ambacho kwanza kitawapata kinamama hapahapa duniani na baadaye katika dhiki kuu na mwisho katika Jehnamu ya moto na ndiyo maana alisema watasema heri wa matumbo yasiyozaa na matiti yasiyonyonyesha.
Mwanamke hakikisha uniombolozea nafsi na kuiambia nafsi yangu mtii Mungu, nafsi yangu usiiname kwa yale unayoaona, hawa watoto wangu si ya dunia, iambie nafsi yako kwamba hawa watoto, hii ndoa, kanisa, vijana,nchi nk ni ya Bwana .
Hakuna hata mmoja wa watoto wangu watakaokwenda Jehnamu , sizai watoto wa kwenda Jehanamu nk.Hakikisha ndani yako ahadi za Mungu zinajaa kwa wingi ili nafsi isitekwe na hivyo ukawa umemruhusu shetani kuvuruga na kuharibu kusudi la Mungu kupitia wewe .
Naamini ujumbe huu utawasidia wamama wengi Kujua namna ya kushughulika na nafsi zao na kuhakikihsa haziwafanyi kutoka kwenye kusudi la Mungu.
Neema ya Kristo na iwe nawe.

1 comment:

  1. Sikuwahi kuamini kitu kama hiki kingeweza kunitokea hadi ndoa yangu ilipokaribia kuisha kabisa.

    Mume wangu alibadilika ghafla. Mwanaume ambaye hapo awali alinipenda na kunijali akawa baridi, asiyejali, na mwenye hasira bila sababu. Aliacha kuonyesha nia katika ndoa yetu, akaniepuka kabisa, na hatimaye akaniomba talaka. Nilivunjika moyo kwa sababu nilimpenda mume wangu kwa moyo wangu wote.
    Mambo yalizidi kuwa mabaya aliponizuia kila mahali — WhatsApp, Facebook, Instagram — kana kwamba sijawahi kuwepo. Nililia kila usiku nikijiuliza nilifanya nini kibaya.
    Siku moja, rafiki wa karibu alinitembelea na kunitambulisha kwa mtu wa kiroho anayeitwa Dkt. Dawn. Kwa kweli, mwanzoni nilikuwa na shaka, lakini niliamua kumweleza kila kitu kwa sababu sikuwa na chochote cha kupoteza.

    Dkt. Dawn alinisomea mambo ya kiroho, na nilishtuka. Alifichua siri kuhusu ndoa yangu na maisha yangu binafsi ambayo hakuna mtu aliyejua. Kila kitu alichosema kilikuwa sahihi 100%. Kisha akafichua kwamba mwanamke mwingine alikuwa amemloga mume wangu. Mwanamke huyu alikuwa akimtembelea mara nyingi, na kwa upumbavu niliamini ilikuwa kuhusu kazi tu.
    Dkt. Dawn alinisaidia kuvunja uchawi na akafanya ibada yenye nguvu ya kurejesha upendo kwa ndoa yangu.
    Kwa mshangao wangu mkubwa, muda mfupi tu baadaye, mume wangu alinifungulia kizuizi mwenyewe na kuanza kunipigia simu na kunitumia ujumbe mwingi, akiniomba nimsamehe na nirudi nyumbani. Mwanzoni nilimpuuza kwa sababu ya maumivu aliyonisababishia, lakini hatimaye alirudi nyumbani akiwa na zawadi na machozi machoni mwake akiomba nafasi nyingine.
    Leo, ndoa yetu ni imara zaidi, yenye furaha zaidi, na yenye amani zaidi kuliko hapo awali. Mapenzi kati yetu yanahisi upya kabisa.
    Kana kwamba hiyo haitoshi, Dkt. Dawn baadaye alinisaidia na ibada ya ujauzito kwa sababu tulikuwa tumejitahidi kwa miaka mingi kupata watoto. Ndani ya wiki 8, nilipata mimba kiasili, na leo tumebarikiwa na wavulana wawili wazuri wenye afya njema.
    Nitaendelea kushukuru milele.
    Ukihitaji: Uchawi wa mapenzi wa kuungana tena na mpenzi wako wa zamani
    . Usaidizi wa kurejesha ndoa
    . Tamaduni za ujauzito za kupata mimba
    . Usaidizi wa kiroho kwa kesi za mahakamani au kupona urithi
    . Mwongozo na ulinzi wa kiroho
    Ninapendekeza sana Dkt. Dawn. Ushuhuda wangu ni wa kweli, na furaha yangu leo ni uthibitisho. WhatsApp yake: +2349046229159

    dawnacuna314@gmail.com

    ReplyDelete