Saturday, April 21, 2012

JIANDAE KUZIKABILI CHANGAMOTO NA KUZITUMIA FURSA ZINAZOKUJA



JIANDAE KUZIKABILI CHANGAMOTO NA KUZITUMIA FURSA ZINAZOKUJA.

 Na: Sanga P.S.
Jiandae kwa sababu mbele yako kuna changamoto zinakuja. Nyingine zimeruhusiwa na Mungu, au wewe mwenyewe kwa kumpa Ibilisi nafasi (Waefeso 4:27). Na bila maandalizi changamoto hizi zinaweza zikaharibu mahusiano yako na Mungu na kupelekea makusudi ya Mungu kupitia wewe kutofanikiwa.
Zaidi nataka ujiandae kwa sababu zipo fursa ambazo Mungu anazileta ili kukufanikisha. Lakini pia zipo fursa ambazo Shetani anazileta na usipokuwa makini nazo zitakuvuruga na kuharibu mahusiano yako na Mungu. Lengo la huu ujumbe ni kukuandaa na kukufunza ujue namna ya kujiandaa kuzitumia fursa ili kukabilana na changamoto mbalimbali zinazokuja.
 Changamoto ni nini?– ni mazingira kinzani, ya upinzani kwenye kila nyanja yanayokuja katika maisha yako. Kwa jina jingine ni matatizo. It is a situation that demands innovativeness, a situation/a trial available to test an organizational/personal capacity/ability.
Kwa hiyo haya ni mazingira/matatizo/vikwazo vinavyojitokeza ili kupima uwezo wa mtu au taasisi/kampuni. Lengo la changamoto ni kukusaidia  uwe mbinifu, mvumbuzi. Changamoto haziwezi kukwepeka kwenye maisha, kwa sababu zimeruhusiwa na Mungu mwenyewe na ndio sehemu ya maisha, soma Mithali 16:4 Ayubu 1:11 Waamuzi 3:1-6   Kumbukumbu 8:1-3
 Fursa–ni nafasi, mlango, uwezo, uwezekano, tukio, muda unaojitokeza/uliopo ili kukuvusha kwenye changamoto inayokukabili.
Fanya maandalizi kwa sababu mbele yako kuna fursa zinakuja ambazo hautakiwi kuzikosa hata moja. Fursa zinakuja ili zikusaidie kukabilana na changamoto ulizonazo. “A big/better opportunity favors the prepared mind”. Hii ina maana fursa inapojitokeza inakuja kuwa jibu la changamoto unayoipitia au itakayokuja kwa hiyo ni vema ukaitumia hiyo fursa vizuri.
Changamoto na fursa ni sehemu ya maisha ya mwanadamu kutoka kwa Mungu. Si watu wengi wanaojua kuzitumia vizuri fursa ambazo Mungu amezileta kwenye maisha yao. Ngoja nikueleze siri hii, kila mwaka una changamoto na fursa zake. Sasa unatakiwa kujiandaa ili kukabiliana na changamoto na kwa kuzitumia fursa  husika.
Mifano ya watu walioshindwa kuzitumia vizuri fursa zao. Soma habari hii katika Luka 19: 41-44. Ukisoma hii habari utaoona jinsi Yesu alivyoulilia mji wa Yerusalemu kwa kushindwa kuzitumia fursa ambazo alizitengeneza kwao lakini wao wakashindwa kuzitumia.
Kosa la Jerusalem ni kutokujua muda wa kujiriwa kwake.. “All this will happen to you because u did not know the time of your salvation”. Kumbuka tulikotoka muda ni fursa Kumbe kuna magumu, mabaya, matatizo yanatupata kwa sababu tu hatujajua namna ya kuzitumia fursa zilizopo mbele yetu.
Hebu tujifunze kutoka kwa nabii Haggai 1:3-11. Soma pia habari hii vizuri. Kosa la watu wa kkipindi cha nabii Hagai ni kusema huu si muda wa kujenga nyumba ya Bwana bali za kwetu. Kwa kuwa walishindwa kuitumia hii fursa wakajikuta kwenye hayo matatizo makubwa ya kijamii na kiuchumi.
Nini maana yake?
Ili uweze kuzikabili changamoto na kuzitumia vizuri fursa zilizopo ni LAZIMA/SHARTI UJIANDAE. Lada niseme hivi maandalizi ni ya LAZIMA ili uweze kukabiliana na changamoto na kuzitumia fursa mbalimbali vizuri.
Zifuatazo ni njia kadhaa ambazo zitakusaidia kujiandaa kukabilina na changamoto zinazokuja mbele yako;
  • Kwa kuwa na malengo. Mithali 29:18.
  • Kwa kuomba bila kukata tamaa (ombeni msije mkaingia majaribuni).
  • Tafuta kujua kusudila Mungu katika maisha yako i.e kwa nini uliumbwa. Ukijua kusudi ni rahisi pia kujua mipango yake katika maisha yako.
  • Ukishajua nini wajibu wako hapa duniani, basi tekeleza kwa bidii, moyo na uvumilivu hayo majukumu. Ongeza ufahamu katika nyanja (field) yako ili upate maarifa ya kukusaidiauwe na ufanisi mzuri zaidi.
  • Kuwa makini na maisha yako (Zaburi 1:1). Hili litakujengea maisha ya nidhamu ili kuhakikisha unakaa kwenye mpango wa Mungu. Kuishi katika mpango wa Mungu kuna gharama zake. Gharama kubwa ni kujikana, ni lazima ujifunze na ukubali kuyahesabu mambo mengine kuwa hasara ili shauri la Kristo liweze kufanikiwa.
  • Weka ndani yako/tafakari neno/sheria ya Bwana usiku na mchana. Hii itakupa kuona njia ikupasayo kuiendea. “Neno la Bwana ni taa ya miguu yangu”.
  •  Jifunze kuwa na muda wa utulivu wa kuomba na kuwaza. Mungu huwa anasema katika utulivu. Utulivu wako ni fursa kwa Mungu kukufunulia FURSA za kukabiliana na changamoto unazozipitia na zinazokuja. 
Mungu akubariki, naamini ukiyaweka haya katika utendaji taratibu utaanza kuona fursa ambazo mungu anazileta kwako ili kukufanikisha. Kumbuka siku zote kwamba mawazo yake ni ya amani, kukupa tumanini siku zako za mwisho.
Nawapenda wale wanipendao na wanitafutao kwa bidii wataniona.
Neema ya Kristo iwe nawe.

No comments:

Post a Comment