KIJANA ZINGATIA HILI, ILI UWEZE KULITUMIKIA KUSUDI LA MUNGU.
“Huu ni waraka maalumu kwa vijana wote ambao bado hawajaoa au kuolewa”.
Na : Sanga.P.S.
Kijana
mwenzangu ninakusalimu kwa jina la Bwana. Katika mwezi huu nina neno
fupi ambalo nimeona ni vema nikushirikishe na wewe juu ya ‘UMUHIMU WA
KUUTAFAKARI MWISHO WAKO UKIUHUSIANISHA NA KUSUDI LA MUNGU JUU YAKO’
Tarehe
29/04/2008 nilifanya maombi maaulumu yaliyolenga kuombea vijana ambao
bado hawajaoa au kuolewa, nikimsihi Mungu afungue milango ya wao kuoa au
kuolewa, kwa sababu wengi wao ninaowasiliana nao bado hawajaoa au
kuolewa.
Katika
kunijibu Mungu alinipa mistari kadhaa na kunifunulia tafsiri yake, nami
nikaandika kwenye kumbukumbu zangu na mwezi huu nimeona ni vema na wewe
nikushirikishe mafunuo haya maana naamini yatakusaidia;
Fungu la kwanza ni, Luka 19:41 – 44.
Soma
fungu hili lote, mimi nitanukuu maneno machache tu. “Alipofika karibu
aliuona mji, akaulilia, akasema, laiti ungalijua hata wewe, katika siku
hii, yapasayo amani … siku zitakuja adui zako watakujengea boma …
watakuangusha chini wewe na watoto wako … kwa sababu hukutambua majira ya kujiwa kwako.
Fungu la pili ni, Isaya 1:2-3
“Sikieni enyi mbingu tega sikio ee nchi … kwa maana Bwana amenena; nimewalisha watoto na kuwalea nao wameniasi, ng’ombe amjua Bwana wake, punda ajua kibanda cha Bwana wake, bali Israel hajui, watu wangu hawafikiri”.
Fungu la tatu (3) ni , Kumbukumbu la Torati 39:29.
“Laiti wangalikuwa na akili hata wakafahamu haya, ili watafakari mwisho wao”.
Katika mafungu haya matatu ya maandiko Roho mtakatifu alinifunulia yafuatayo;
*Kwanza
alisema, usifikiri hao watu unaowaombea siwajibu. Wengi nilishawajibu,
lakini wengine kwa sababu zao binafsi, wazazi wao, Viongozi wao n.k hawajatii
wazo langu juu yao/mapenzi yangu juu yao. Mimi ni Mungu ninayeangalia
kesho/mwisho wa mtu/watu na lolote ninalofanya nimeliona mwisho wake. Sasa kwa kuwa hawa vijana wamekataa wazo langu kwa kutofikiria mwisho wao na kusudi langu kupitia wao na ndoa zao, basi, hakika ndoa zao zitakuwa na shida na baadhi yao wataniacha kabisa.
*Pili, Mungu kwa uchungu sana anataka mbingu na nchi zisikie na zijue kwamba watoto wake ambao amewalisha na kulea wamemuasi.
Watoto hao wameshindwa kujifunza kupitia ng’ombe na punda, na tatizo
lao ni kutokufikiri. Hii ina maana kutokufikiri kwao kumepelekea wao
washindwe kumjua Mungu. Kinamuuma sana Mungu, anapoona watu aliowaokoa na kuwafundisha au kuwaonyesha njia wapasayo kuiendea wanakataa kwenda katika njia yake.
Zaburi 32:8 anasema “Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea, nitakushauri jicho langu likikutazama”.
Sasa kitu kinachomuumiza ni pale anapowaonyesha watu njia yake au
mapenzi yake kwao kuhusu wake/waume zao watarajiwa na akina nani halafu
wao wanashindwa kutii. Licha ya kuwaonyesha au kuwajulisha mapenzi yake
bado wameasi.
Ndugu
kijana mwenzangu, natamani Mungu alete kitu hiki ndani yako kwa uzito
ule ule aliouleta ndani yangu, ili usije ukakataa wazo la Mungu kwako na
ukamkosea hata kuikosa mbingu kwa sababu tu ya mke au mume.
Sasa fanya yafuatayo ili kukaa katika mapenzi yake;
(a) Jifunze
kutafakari mwisho wako, ukijua ya kwamba mwisho wako uko mikononi mwa
Mungu. Na kwa sababu hiyo maamuzi yoyote unayoyafanya ni lazima, na si ombi umruhusu Mungu akuongoze ili uenende katika njia zake.
(b) Haijalishi
kwa jinsi ya mwili huyo mtu ana upugnufu/udhaifu wa aina gani kwa
mtazamo wako, maadam una uhakika ni mtu wa mapenzi ya Mungu uishi naye,
basi usijaribu kukataa huyo mtu kwa sababu Mungu ameona unakokwenda
kukoje na huyo aliyemleta ndiye ambaye mtafika naye mwisho wenu.
(c) Hivyo basi wazo lolote/kijana/mtu yoyote anapokuja kwako kutaka muoane na ndani yako unaona hakika ni mtu wa mapenzi ya Mungu, basi kabla
hujakataa kwa sababu zako binafsi, kaa chini utafakari, mhoji Mungu kwa
maswali yanayokutatiza. Unapokwenda mbele za Mungu siku zote yeye ni
mwaminifu atakupa majibu ya msingi na nina kuhakikishia unapotii uongozi
wa Mungu kuna baraka za ajabu sana. Lakini unaposhindwa kutii itakugharimu kuliko unavyofikiri.
*Mungu
anapokuonyesha/anapokupa mke au mme hamleti kwako kwa lengo la
kukukomoa, bali anakua ameangalia kwanza kusudi lake, changamoto
zilizopo mbele yenu na umbali mnaotakiwa kusafiri kwa pamoja kisha ndio
anawaunganisha kwa kukupa mtu (mke au mume) ambaye anajua ukiwa naye
hakika kusudi lake litafikiwa na mtaweza kuzikabili na kuzishinda
changamoto zote zitakazojitokeza.
Hivyo
mwenzi yoyote unayempata kama una hakika katoka kwa Mungu hata kama ana
mapungufu gani kwa fikra zako au wazazi au dhehebu lako mimi nakushauri
usimkatae, kwa sababu kwa huyo wewe utaweza kulitumikia shauri la
Bwana.
Aliye na masikio na asikie lile ambalo Roho wa Bwana asema na vijana.
No comments:
Post a Comment