UNAJIFUNZA NINI KUPITIA HUDUMA YA ANANIA NA BARNABA KWA PAULO?
Na; Patrick Samson Sanga.
Utangulizi;
Nakusalimu katika jina la Bwana, mpenzi msomaji.
Katika nyanja hii, leo nimeona ni vema tushirikishane kile ambacho Mungu alikifanya kwa Paulo kupitia huduma ya Anania na Barnaba. Si watu wengi sana wanofahamu nafasi ya Barnaba na Anania kwa Paulo, kwanza mtu mwingine ukimuuliza unawafahamu kina Anania wangapi kwenye kitabu cha Matendo ya mitume wangekutajia Anania, mume wa Safira tu yule aliyeuawa kwa kuiba sadaka ya kiwanja na mkewe.
Nafasi ya Anania na Barnaba kwa Paulo.
Matendo ya Mitume 9: 10 -19 “kulikuwa na Mwanafunzi huko Dameski, jina lake aliitwa Anania……..
Matendo ya Mitume 9:27 inasema “ na Barnaba akamchukua—-‘
Watu
wengi sana wanamfahamu vizuri Paulo na kumsifu kwa kazi nzuri
aliyoifanya, hata mimi nuaungana na watu wenye mtazamo huo. Lakini si
watu wengi pia wanaojua kwamba kazi aliyoifanya Paulo ni matunda ya
uaminifu na utiifu wa Anania na Barnaba kwa Mungu wao. Watu wengi
wanafikiri Paulo baada ya kuokoka tu, hapo hapo alianza huduma, si kweli
wanatheolojia wansema inawezekana Paulo alikaa miaka 14 kwanza ndipo
akaanza huduma. Na ukisoma vizuri kitabu cha wagalatia utagundua Paulo
alikaa miaka 17 tangu kuokoka kwake na ndipo huduma yake ikapata kibali
machoni pa mitume na watu wote.
Sasa
katika kipindi hiki cha mpito licha ya kuendelea na huduma, Paulo
alikuwa akifunzwa au akielekezwa kitu cha kufanya kupitia watu
mbalimbali na hasa Anania na Barnaba. Anania ndio
mwanafunzi wa kwanza aliyejenga msingi wa huduma ya Paulo, hii ina maana
Anania angekosea huenda huduma ya Paulo ingesumbua pia.
Vivyo
hivyo na Paulo alipokwenda Yerusalemu wanafunzi wote walimtenga.
Barnaba ndiye aliyemchukua akamtia moyo na kumfariji na kisha
akaitambulisha huduma yake kwa mitume na wanafunzi wengine na ndipo
Paulo akapata kibali na uhuru wa kufanya huduma hiyo. Unaweza ukaona
kama ni kitu kidogo lakini katika ulimwengu wa roho hawa watu waliweka
alama kubwa sana na ndio maana hadi leo mimi na wewe tunabarikiwa na
nyaraka za Paulo.
Jifunze yafuatayo kupitia ndugu hawa.
Moja,
usiidharau nafasi yako mbele za Mungu, kumtumikia Mungu si mpaka
usimame madhabahuni ufundishe maelfu ya watu. Wapo waliopewa kusimama
madhabahuni lakini pia wapo waliopewa kutengeneza wale watakaosimama
madhahuni. Using’ang’anie wajibu usiokuwa wa kwako. Kila mmoja katika
mwili wa Kristo ana wajibu wake.
Paulo
amejulikana sana lakini mbele za Mungu Anania na Barnaba wanaheshima
zao kubwa zaidi kwa kukubali maagizo ya Mungu juu ya Paulo. Haijalishi
watu wanaidharau kiasi gani huduma yako, uwe na uhakika Mungu
anaithamini sana kazi yako. Huenda wanadamu wasikutukuze au kuona
umuhimu, mchango wako katika ufalme wa Mungu bali uwe na uhakika pia
Mungu ameiona na kuiheshimu sana kazi yako. Kwa Mungu Anania na Barnaba
wana nafasi ya kwanza kuliko Paulo kwa sasbabu wao walikuwa walimu wa
Paulo kiroho. Na neno linasema mwanafunzi hampiti mwalimu wake.
Tekeleza
wajibu wako na Bwana Mungu atakubariki katika hilo. Usitafute
kuonenkana na watu, tambua kwamba Mungu yu pamoja na wewe. Siku zote
zote lenga kutengeneza watu watakaotengeneza na kubadilisha maelefu ya
watu. Usibakie kung’anga’nia madhabahu isiyo ya kwako kwa kugombana na
wachungaji. Kama Mungu amekuletea hata mtu mmoja kama Anania,
tekeleza wajibu wako vema kwa kumfunza huyo. Nani ajuaye huenda atakuwa
mfano wa Paulo kwa kizazi cha leo. Sasa ni vema ukae kwenye nafasi yako
na ndipo ufanisi wako utakuwa mzuri zaidi. Kadri unavyokuwa mwaminifu
kwa huyo mmoja ndivyo Mungu atavyowapitisha na wengine wengi kwako upate
kuwajenga na kuwafundisha njia ya Kristo ili waje kuwa watumishi wazuri
wa kesho.
No comments:
Post a Comment