Jitambue Ya Chris Mauki...FAHAMU JINSI YA KUISHUHULIKIA NA KUIPUNGUZA HOFU--Part 1
Hofu
na mashaka ndio adui namba moja anayefilisi nguvu au nishati ya mwili
wa mwanadamu kwa haraka kuliko kitu kingine chochote kile. Wengi wameathiriwa katika maisha yao ya kielimu, kiafya, kijamii, kikazi na hata kiuchumi kwasababu ya hofu au mashaka.
Wengi wameshindwa kufikia malengo na ndoto zao katika Maisha kwasababu ya hofu na mashaka.
Mara
tu hofu na mashaka yanapoota ndani ya mtu hudumu kwa muda mrefu huku
yakileta uharibifu mkubwa katika nafasi, akili, na maendeleo ya mtu huyo
kwa ujumla. Makala au mada hii
itakuwezesha kufahamu kwa kiasi kikubwa mambo unayoweza kufanya ili
kuondokana au kupunguza athari za hofu na mashaka na pia kuweza kutoa
msaada kwa yeyote anayepitia tatizo hili kwa wakati fulani.
Hofu ni mjumuiko wa kujali kusiko na sababu yoyote (unnecessary concern) au kusiko na maana yoyote juu ya nafsi au utu wa mtu. Tunasema hakuna sababu wala umuhimu wowote kwa sababu kujali huku kumejengwa katika misingi ifuatavyo
- Mtu kujali sana au kuweka mawazo sana katika vitu ambavyo viko nje ya uwezo wake.
- Mtu kuanza kusikitikia mambo yajayo badala ya kujipanga na kujiandaa kuyakabili pale yatakapo wadia.
- Kuweka
msisitizo zaidi katika jambo moja na kuyasahau mengine. Anayehofu
hudhani kwamba ikiwa kile anachokiwekea msisitizo kitashindikana, basi
kila kitu kitakuwa kimeharibika.
- Mtu kushindwa kutumainia imani aliyonayo juu ya ufanisi wa jambo fulani. Hofu yake katika jambo fulani huizidi imani aliyonayo na kwahivyo hali ya kushindwa kuonekana dhahiri zaidi kuliko hali ya kushinda.
Kwasababu hofu hujengwa katika fikra zisizo na maana wala uhalisi wowote, basi njia ya kuiweza hofu hiyo ni lazima iwe kwa kutumia fikra zenye maana na uhalisi ili kuushinda uwezo wako wa kufikiri kushindwa.
Yafuatayo yatakusaidia kukuwezesha kupunguza kiwango cha hofu katika Maisha.
1. Jiulize swali “Je nini kinachoniangamiza?”
Hofu ni kitu kinacho angamiza, tena huangamiza kwa viwango na hatua tofauti. Ngoja nijaribu kukupa mfano wa maelezo.
Hofu kwa lugha ya kingereza ni “worry” neno “worry” limetokana na lugha ya Kidachi lenye maana ya “Worgen”. Maana
ya neno “worgen” ukiipeleka moja kwa moja katika lugha ya kingereza
humaanisha “strangle”. Maana ya neno “strangle” kwa lugha ya kiswahili
ni “Kunyonga kwa kamba”. Sasa yamkini hapa unanielewa kwanini ninasema hofu huua au kuangamiza.
Uzuri ni kwamba, hofu haiangamizi pasipo kutoa tahadhari kabla, baadhi ya tahadhari zinazotolewa katika mchakato wa kuangamizwa na
hofu ni pamoja na hamaki za mara kwa mara, mvi za mapema, baadhi ua
upele fulani wa ngozi, vidonda vya tumbo (ulcers), matatizo ya kukosa
usingizi, kuhitaji kwenda haja ndogo mara kwa mara n.k.
Swali
hili la “ni nini kinachoniangamiza?” litakuwezesha kujitathmini wewe
mwenyewe. Katika kulijibu swali hili utaweza kutathmini kwa kujiuliza
kuwa “Ni nini katika maisha yangu ambacho nimekipa kipaumbele zaidi
kuliko afya yangu na Maisha yangu? Maana ya swali hili ni ukweli kwamba
kama unahofu katika jambo fulani maana yake hilo jambo au hicho kitu
umekipa umuhimu au uzito usiostahili kuliko maisha yako. Je ni jambo gani au kitu gani umekipa umuhimu au uzito usiostahili katika maisha yako. Je ni kazi yako?, Je ni elimu yako? Je ni ujenzi wa nyumba? Je ni kibali kwa watu? Je ni watoto wako au mwenza wako? Je
ni malipo ya mkopo uliouchukua? Kumbuka haitakufaidia wala kukuongezea
chochote kwa kujiua ukikiwaza hicho kitu, mwisho wasiku mwenye hasara ni wewe.
Hata mwisho kama hautapoteza maisha yako lakini ukadhoofisha afya yako, faida yake nini nini? Na afya yako ikipotea, nini tena utakifanya kuyanufaisha maisha yako?
Kama hofu yako ni kwenye kupata kibali machoni pa watu wanaokuzunguka, labda ofisini, chuoni, mtaani nk. Kumbuka
kuwa watu hao wala hawatajali au kukukumbuka pale utakapokuwa unaugulia
wodini au nyumbani kwako kisa ni magonjwa yanayohusiana na hofu.
Labda mfano huu waweza kukusaidia zaidi kuelewa ninacho maanisha.
Mtu
mmoja kijana alimuuliza swali mwanafalsafa (philosopher) mmoja akisema,
“Nini kinachokushangaza sana kwa huyu kiumbe binadamu?”
Mwanafalsafa alijibu “Ninamshangaa sana kiumbe mwanadamu kwa sababu hupoteza afya yake kwa kiasi kikubwa sana akitafuta pesa, na baadae hutumia pesa yake yote akiitibu au kujaribu kuirejesha afya yake iliyo potea katika hofu za Maisha. Kwa
kuihofia kesho yake, mwanadamu huyu ametumia muda wote wa sasa
akijiandaa na hiyo kesho, na matokeo yake, kwa kuichosha sana afya yake
ameshindwa kuifurahia leo yake na hata hiyo kesho yenyewe huiona kwa
taabu sana” (Mwenye ufahamu na afahamu).
1. Acha kuyapa mawazo yako au mitazamo yako umuhimu usiostahili
Hofu, woga na hamaki za mara kwa mara ni alama kwamba unayapa mawazo, fikira na mitazamo yako umuhimu usiostahili. Maana
yake ni kwamba kila unaloliwaza au kulifikiri unalichukulia kua ni
halisi, ingawa maranyingine ukweli ni kwamba unavyowaza sivyo.
Hakuna ukweli wala uthibitisho kuwa kila unacho kiwazakitatokea.
Hizi twaweza kuziita fikra laini, pale ambapo unadhani kuwa kila unachowaza kitatolea. Mtu
mwenye ukichaa, akiwaza kuwa kuna mtu anataka kumpiga risasi atakimbia
huku na huko kujificha. Wakati ukweli ni kwamba hakuna kitu kama hicho.
Wewe sio kichaa, kwanini uweke vyote unavyoviwaza kama vile ni dhahiri? tena hususani vile vitu vibaya?
Tabia sugu nyingi walizonazo watu husababishwa na fikra, vile wanavyowaza. Usiruhusu mawazo yako yakufanye mtumwa. Mawazo ya kitaalam yanaonyesha kwamba kama ukiweka mawazo yako sana katika kitu fulani, inaweza kuishawishi tabia au utendaji wako katika hali ambayo yaweza kuanza kufanya hofu zako kuanza kuwa kweli. Ni kwasababu hii ndiyo maana, unashauriwa kuweka mawazo na fikra zako zote kwenye vitu ambvyo ni vya maana.
2. Usijiogopeshe kwa vitu ambavyo hutokea kwa nadra sana
Njia
bora ya kuyatengeneza mawazo yetu yanayofikiri sana juu ya hatari
ambazo kutokea kwa nadra sana ni kwa kuwaza kuwa wewe hautakuwepo pale
hatari hiyo itakapo tokea katika eneo hilo, na hivyo haitakuathiri.
Kwanini uwaze kwamba wewe una bahati mbaya sana na vyote vibaya vitakapotokea vitakukuta wewe tu. Najua inawezekama kabisa lakini nafasi za kuwezekana huko ni ndogo sana. Mfano. Kwanini uwaze kuwa unapotembea msituni peke yako, mti unaweza kukuangukia. Au
unapokukwa kwenye ndege au meli, ajali yaweza kutokea, au hata
unapokuwa safarini kwa gari, jiulize mabasi mangapi yametoka kule
unakotokea na kufika salama kule unakokwenda bila shida yeyote, wewe je
huwezi kuwa mmoja wa waliokuwa salama?
Kuna
mambo mengi ya kuogopesha yanayotokea katika maisha yetu ya kila siku,
na kama ukiogopa na kuhofu kila kitu na kutofuata ushauri unaotolewa
hapa, basi kila siku utatembea na kuishi kwa hofu tu.
No comments:
Post a Comment